Kwanini TGVS?

Kwa nini kuwe na Huduma hii ya Sauti Ya Injili?
Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote kama ushuhuda kwa mataifa yote, na ndipo ule mwisho utakapokuja.
• Injili lazima ihubiriwe ulimwenguni pote ndipo Yesu Atakuja Tena ( Matayo 24:14).
• Ulimwengu hauwezi kusikia Injili pasipo mhubiri (Warumi 10:14).

Katika (Warumi 10:17), mtume Paulo anasema “Imani huja kwa kusikia, na kusikia huja kwa neno la Mungu”.
• Sauti ya Injili ipo ili kutoa mhubiri / wahubiri wa Injili.
• Sauti ya Injili ipo ili kuwaonya watu kuhusu hatari za kufuata “Injili Nyingine” (2 Wakorintho 11: 4),
• Sauti ya Injili ipo ili kuhubiri Ujumbe wa Malaika Watatu (Ufunuo 14: 6-13, Ufunuo 18: 1-4)
• Sauti ya Injili ipo ili kuhamasisha watu kiiimani kwa njia ya Neno la Mungu.

Katika (Mathayo 4: 4) Yesu anasema “Mtu Hataishi Kwa Mkate Tu, Ila Kwa Kila Neno Litokalo Katika Kinywa Cha Mungu”.
• Yesu ni Neno (Yohana 1: 1).
• Yesu anasema kwamba neno lake ni KWELI (Yohana 17:17), tena ni UZIMA (Yohana 6:63).
• Kumfahamu Yesu ni kuwa na UZIMA WA MILELE (Yohana 17: 3).
• Sauti ya Injili ya ipo kwa ajili ya kuwasaidia watu kumjua Yesu kupitia kurasa za Biblia Takatifu.

Ninawezaje Kushiriki?
• “SOMA” (Isome Biblia), “ELEWA” (Tafuta uelevu wa aya unayoisoma),”SHUHUDIA” (mwambia mwingine kuhusu Kristo Yesu)
• Gundua baadhi ya mahitaji ya huduma hii na jinsi gani unavyoweza kusaidia.
• Gundua uzuri wa YESU na Neno Lake kwa kusikiliza ujumbe huu mwenyewe.
• Toa msaada wako wa hali na mali ili kuboresha zaidi hii Huduma ya Injili.
• Soma ushuhuda wa watu kama wewe ambao wamekwisha barikiwa na Huduma hii.
• Tueleze jinsi huduma hii ilivyoleta badiliko fulani katika maisha yako.
• Mwambie jirani, rafiki, na familia yako kuhusu hii Huduma ya Injili.

Wchungaji; Wahubiri; Wainjilisti; Waimbaji
• Bado tunahitaji wahubiri wengi walio na shauku kama yetu, ili tufanye kazi hii pamoja.
• Kama Bwana anuzungumza nawe, Tafadhali toa Masomo yako ili tuyapakie (upload) Hapa.
• Tunahitaji pia Wahariri, Waandishi, Watafsiri; Wafadhili; na kadhalika.
Bwana akubariki ndugu msomaji/ msikilizaji katika kazi Yake njema.
• Mtuombee pia kila siku ili tufanikishe na kubariki wengi katika shughuli hii njema na takatifu, panapo nafasi.
• Kumbuka maneno ya Kristo: “Mavuno ni mengi, lakini watendakazi ni wachache.”
• OMBI LETU: “Ee Mwokozi Yesu, tufanye kuwa sehemu ya watendakazi Wako waaminifu”Katika Jina la Yesu Kristo, Amina!

KARIBUNI SANA WAPENDWA, BWANA ATUBARIKI SOTE.