January 9, 2017
BIBLIA: “Soma, Elewa, Shuhudia”
KIPINDI CHA MAOMBI NA IBADA YA ASUBUHI
- Mada: Ufalme wa Mbinguni
- Kitengo: Chumba cha Maombi
- http://tgvs.org/archives/2204
- Jumatatu: January 9, 2017
SAUTI YA INJILI:
- (Ebu sikiliza Ahadi/ Sauti ya Mungu ikinena nawe Asubuhi ya Leo)
2 Corinthians 6:17–18
- 17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
- 18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike.
CHANGAMOTO TUNAZOZIOMBEA LEO HII.
- UINJILIST: Radio Morning Star & Staff wote
- DEVON: Tumuombee Mungu aingilie kati shida kuu inayomsibu
- WANAKIKUNDI: Ujazo wa Roho Mtakatifu, Upendo, Umoja, Msamaha, Utakaso, na Uaminifu wa Members wote wa kikundi hiki, ili wawe waaminifu katika Kuomba na Kuombea wengine pia.
- MSHITU: Anaendesha mahibiri kwa njia ya Radio, na tayari watu wanne (4) wamejitokeza kubatizwa; tuzidi kuombea huduma yake.
- OGETO: Ana Job Interview leo hii, tumuombee ili mambo yaende sambamba, kama ni mapenzi ya Mungu, achaguliwe katika candidates wengi waliopelekamaombi ya kazi.
- UTII WA NENO– “Lakini iweni watendaji wa NENO, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu”. Tutafakari Maonyo Ya Yesu; Tuungame na Tutubu dhambi zetu, Tujiweke tayari daima: “Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu”. (Yakobo 1:22; Luka 21:36)
UNGANA NASI KWA AJILI YA MAOMBI
- Kila Siku Alfajiri: Hapa katika kikundi
- Siku 10 za Maombi: January 11–21; 2017
- Ombea jirani yako: changamoto mbalimbali zinazowasibu
- Ombea nafsi yako: utubu, uokolewe, uingie mbinguni
- Ombea viongozi wa serikali: Hekima, Amani, n.k.
- Ombea viongozi wetu wa kanisa: Bwana awatangulie
- Ombea huduma hii ya Sauti Ya Injili SDA
- Ombea mchakato wa Injili Ulimwenguni kote (Matayo 28:19-20)
- Ombea mtu mmoja atakayesikia kweli hizi za Biblia akapate kuokolewa.
- Jiandae kukutana na Mungu Wako. “Ujiweke tayari kuonana na Mungu wako, Ee Israeli”; (Amosi 4:12).
TUNAKARIBISHWA KUFANYA YAFUATAYO:
- Kuweka Maombi (Maandishi/ Sauti)
- Kutoa ushuhuda wa Matendo makuu ya Mungu wetu.
- Kuandika Mahitaji/ Maombi/ Changamoto mbalimbali zinazokusibu
ANGALIZO:
- Kama nimesahau ombi la mtu fulani, naomba uniinbox, ili tuliweke.
- Mahitaji yatakayo orodheshwa leo, yatakusanywa na kuombewa kesho Asubuhi.
BWANA ATUBARIKI SOTE.
Matayo 26:41
“Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.
Sauti Ya Injili SDA © 2017. Haki zote zimehifadhiwa.