01-Maandiko Matakatifu
MFULILIZO WA MASOMO MAFUPI YA INJILI
- Mhutubu: Angelo Nyamtema, MD, PhD
- Ifakara-Tanzania, East Africa
MAANDIKO MATAKATIFU
UFUPISHO WA SOMO
Katika Biblia Takatifu tunasikia maneno haya:
- “Heri asomaye na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo; kwa maana wakati u karibu” (Ufunuo 1:3)
Katika 2 Timotheo 3: 16-17, mtume Paulo akivuviwa na Mungu Roho Mtakatifu, anaandika akisema:
- “16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; 17 ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”
Je, rafiki unayachukuliaje maandiko Matakatifu ya Mwenyezi Mungu? Je, wafahamu kua katika maandiko hayo kuna maonyo, mafundisho, mwongozo, n.k.?
Ebu, chukua wasaa kidogo kusikia huyu mtumishi wa Bwana akituletea somo: MAANDIKO MATAKATIFU.
Bwana atubariki sote.